Habari za hivi Punde

SHIBUDA AMNUSURU NAIBU WAZIRI WA KILIMO NA CHAKULA KUTAKA KUSHUSHIWA KIPIGO NA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA.

Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Godfrey Zambi juzi nusuru apate kipigo kutoka kwa wakulima wa pamba katika kijiji cha Marekano Kata ya Kadoto Wilayani Maswa Mkoani Simiyu wakati alipowatembelea wakulima hao, kwa kile kilichodaiwa kupewa majibu yasiyo ridhisha juu ya Mbegu za Quton.

Wakati akiotoa majibu kwa wakulima hao ambao waliokusanyika gafla katika kituo cha kukusanyia pamba alichokitembelea kukagua mizani inayotumika kupima zao hilo, wakulima hao walianza kumzomea Naibu waziri huyo wakati akiongelea Mbegu hizo pamoja na bei ya pamba.


Wakulima hao walitaka kujua hatima yao juu ya kupewa fidia kwa wale ambao walitumia mbegu hizo, ambazo haizkuota na kuwasababishia hasara kubwa, ikiwa pamoja na kutaka kujua mipango iliyopo ya serikali kuwadhibiti wafanyabishara wanaowaibia kupitia mizani ya Digital.

Wakati akitoa majibu hayo Zambi alianza kuzomewa na kutaka kupigwa na wakulima hao, baada ya kutoridhika na majibu yaliyokuwa yakitolewa na kumtaka aondoke katika eneo lao kwa kile walichodai kuwa serikali imeshindwa kuendeleza zao la pamba.

Wakiongea kwa hasira wakulima hao walimtaka naibu waziri kuifuta bodi ya pamba (TCB) kwa kile walichokidai kuwa wamekuwa wakiteseka na kuangaika bila ya kuhurumiwa katika kupanda, kuvuna hadi kuuza zao hilo.

Walisema bodi ya pamba imekuwa chanzo cha zao la pamba kuporomoka pamoja na kusababisha umaskini mkubwa kwa wakulima wa zao hilo, kwa kuwanyonya katika bei yake ikiwa pamoja na kuwaletembea mbegu mbovu.

“tunaomba uondoke hapa…hatukutaki hata kidogo..serikali mmetonyonya sana wakulima wa pamba na tunaomba ukiondoka hapa ondoika na bodi ya pamba na mbegu hizo za Quton hatuzitaki hata kidogo” Walisema wakulima hao.

Wakati wakulima hao wakimfukuza Naibu Waziri Mbunge wa Bariadi Magharibi John Shibuda aliwatuliza wakulima hao na kuwazuia wasimpigi wazari ambapo aliwaondoa katika eneo ambalo waziri alikuwepo na kuwapeleka mbali.

0 Response to "SHIBUDA AMNUSURU NAIBU WAZIRI WA KILIMO NA CHAKULA KUTAKA KUSHUSHIWA KIPIGO NA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.