Habari za hivi Punde

UPATIKANAJI WA DAMU SALAMA MKOANI SHINYANGA BADO KUNACHANGAMOTO


Wito umetolewa na  chama cha msalaba mwekundu mkoani Shinyanga  kwa wananchi kujitokeza   kuchangia damu salama  ambapo  mazoea yaliyojengeka  ni pale wanapopatwa  na mgonjwa  nayehitaji damu ndipo huchukua jukumu la  kujitokeza  kuchangia damu hiyo bila kuwa na hofu yoyote.
Hayo yalisemwa na mratibu wa damu  salama wa  chama hicho mkoa  Anna Lusana  wakati alipokuwa akiongea na mwandishi wa  BLOG HII  ofisini kwake,huku akieleza kuwa  kwa mwaka jana  waliweza  kupata jumla ya uniti  4145 za damu salama   sawa na asilimia 80 ikiwa lengo ni kufikia   uniti 5000.
Lusana alisema kuwa  jamii  inauelewa juu ya kuchangia damu ila bado wana hofu kubwa ya kupimwa maambukizi ya virusi  sanjari na imani potofu waliyonayo  kwa baadhi, ambapo uchangiaji wa damu   mara nyingi wamekuwa wakijitokeza  pale  wanapokuwa na mgonjwa anayehitaji kuongezwa damu salama,pia changamoto nyingine kutegemea hasa wanafunzi mashuleni.
“Imani potofu  iliyopo kwa baadhi ya wananchi hasa maeneo ya vijijini  kuwa wakitoa damu wataugua,hofu ya kupimwa maambukizi ya virusi ikiwa pia hutegemea zaidi wanafunzi wa shule ya sekondari  waliofikisha umri wa miaka 18 nao ni wachache ikiwa wengi wao hawajafikisha umri huo, na mazoea yaliyopo mtu kutoka damu mpaka awe na  mgonjwa mwenye mahitaji ya kuongezwa damu salama na kujitokeza hiyo ndio changamoto” alisema  Lusana.
Lusana alisema kuwa upatikanaji wa damu salama mara nyingi wamekuwa na vigezo kwa kuangalia historia ya  maradhi ya mtu anayetaka kujitolea damu asiwe ametibiwa  muda wa miezi mitatu na kuna makundi ambayo ni  wale wanaojitolea kwa hiari, wenye wagonjwa   wa mahitaji  ya kuongezwa damu salama,  pamoja na kwenye mikusanyiko  ya watu kama minadani  ambayo   upatikanaji wake asilimia kubwa  damu yake siyo salama kwenye kundi hilo.



0 Response to "UPATIKANAJI WA DAMU SALAMA MKOANI SHINYANGA BADO KUNACHANGAMOTO"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.