Habari za hivi Punde

WANANCHI WA JAMII YA WAFUGAJI KIJIJI CHA MBALA CHALINZE WAPATA UHAI.


 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete akiongozana na akina mama wa jamii ya kimasai waliobeba maji waliyoyateka baada ya mbunge huyo kuzindua kisima cha maji katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, Bagamoyo mkoani Pwani jana. Kisima hicho pamoja na lambo la kunyweshea mifugo vimejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. Kushoto ni Kiongozi wa mradi huo, Joseph Chagama na nyuma yake ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Ridhiwani Kikwete akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kisima hicho. Kushoto ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana.
 Ridhiwani akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa jamii ya kimasai baada ya kuzindua kisima hicho.
 Mama mwingine wa Jamii ya Kimasai akitwisha ndoo ya maji na Ridhiwani Kikwete

 Ridhiwani Kikwete akifungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua lambo la kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mbala kinachokaliwa kwa asilimia kubwa na jamii ya wafugaji
 Ng'ombe wakitoka kunywa maji kwenye lambo hilo

0 Response to " WANANCHI WA JAMII YA WAFUGAJI KIJIJI CHA MBALA CHALINZE WAPATA UHAI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.