Habari za hivi Punde

WAZIRI HAWA GHASIA KULIKONI KWA WATUMISHI HAWA WA SERKALI ZA VIJIJI WILAYANI MEATU?

MADIWANI  wa Halmashauri ya wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wamewafuta kazi  watendaji  watano  wa serikali za vijiji  na mmoja mtendaji wa kata  kwa kile kilichodaiwa utoro kazini  bila kutoa taarifa pamoja na kuzarau viongozi wa ngazi za juu ndani ya Halmshauri hiyo.



Akitoa azimio la Madiwani katika kikao cha Baraza la halmashauri kilichofanyika  katika ukumbi wa Halmshauri hiyo Mwenyekiti wa baraza hilo Pius Machungwa alisema madiwani wameazimia kuwafukuza kazi watumishi hao.



Machungwa alisema kuwa kutokuwepo kwa watendaji hao kwa muda mrefu katika maeneo yao ya kazi imesababisha wananchi kushindwa kuhudumiwa ipasavyo hasa kutatua kero mbalimbali zinazowakabili ndani ya vijiji vyao.


“wamekuwa watoro kwa kipindi kirefu..lakini pia tulishawandikia barua za onyo ili kuweza kujirekebisha wamepuuza barua zetu na za waajiri wao hivyo baraza la madiwani limeamua kuwafuta kazi watumishi hawa kwa makosa hayo”


Alibainisha kuwa Katika vijiji walivyokuwa watendaji hao kulionekana miradi ya maendeleo kusimama kwa muda mrefu bila ya kuendelezwa kutokana na kukosekana kwa usimamizi wao hali iliyosababisha miradi hiyo kutelekezwa na makandarasi.


Waliofukuzwa kazi ni pamoja na Shiwa Charles ambaye ni mtendaji wa kata ya Bukumbi,Paul Lalida mtendaji wa kijiji cha Nata,John Joseph mtendaji wa kijiji cha Baluli na Richard Matanga ambaye ni mtendaji wa kijiji cha Witamhinya.


Mwingine ni Charles Makaranga ambaye ni mtendaji wa kijiji cha Mwaga huku Halmashauri hiyo ikimpa onyo kali Afisa ugavi msaidizi Emanuel Marwa  kwa kosa la kudharau viongozi wa ngazi za juu pamoja na watumishi wenzake.


Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amewataka watendaji wa vijiji na kata kusimamia kesi za migogoro ya mipaka ya shule za msingi na sekondari ili kuweza kuhakikisha maeneo yenye migogoro yanatatuliwa.



0 Response to "WAZIRI HAWA GHASIA KULIKONI KWA WATUMISHI HAWA WA SERKALI ZA VIJIJI WILAYANI MEATU?"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.