Msikiti wa Mtambani uliopo Kinondoni jijini Dar es Saam uliungua kwa mara ya pili leo. Msikiti huo uliungua kwa mara ya kwanza mnamo Agosti 13, 2014 katika ghorofa yake ya juu na kuteketeza eneo kubwa ambalo hadi sasa bado halijanza kufanyiwa ukarabati.
Leo hii moto huo inasemekana ulianza majira ya saa sita na nusu mchana katika moja ya chumba ambacho wanafunzi wa kidato cha nne wa kike wamekuwa wakipiga kambi ya kujisomea ikiwa ni katika maandalizi ya kukabiliana na mtihani wao wa taifa utakaofanyika baadaye mwaka huu.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kanda ya Kinondoni Camilius Wambura amethibitisha jambo hilo na kusema kuwa hadi wanafika eneo la tukio chanzo bado hakijafahamika, na kwamba chumba ambacho moto ulianzia ni cha wasichana ambamo magodoro manne yameungua.
“Katika janga la moto uliounguza madarasa mwezi uliopita Jeshi la Polisi iliunda timu
ambayo ilikuwa ikichunguza chanzo cha moto huo hivyo na sasa timu
hiyohiyo itaendele na uchunguzi wake kwa kuunganisha matukio haya
mawili” alisema Wambura.
Wakizungumza bila ya kutaja majina yao kina mama wa msikitini hapo wao walisema kwamba
“ Sisi tulikuwa msikitini tunasoma qurani wakati tukivuta muda wa sala
ya Ijumaa ndipo tukasikia sauti za moto moto na kuona upande wa wanaume
wakikimbia huku na kule kwa taharuki hivyo chanzo hasa cha moto sisi
hatukijui."
Waumini wa msikiti huo walifanikiwa kuuzima moto huo na kusali swala ya Ijumaa kama kawaida.
Usalama ukiwa umeimarishwa
Kasi ya kuzima moto ikiongezeka
Gari la zima moto likiwa linafanya kazi ya kuzima moto huo
0 Response to "MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI WAUNGUA KWA MARA YA PILI WAUMINI WASHANGAZWA."
Post a Comment