Habari za hivi Punde

WAJUMBE WA BARALAZA LA MAMALAKA MIJI MIDOGO WAIOMBA SERIKALI KUWALIPA KIINUA MGONGO.

SERIKALI imeombwa kuangalia uwezekano wa  kuwalipa kiinua mgongo
wajumbe wanaounda Mabaraza ya Mamlaka ya Miji Midogo hapa nchini pindi
wanapomaliza muda wao kama ilivyo kwa madiwani katika halmashauri za
wilaya.

Rai hiyo ilitolewa jana na wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo katika
Wilaya ya Maswa  mkoani Simiyu kwenye  kikao cha baraza la mamlaka
hiyo kilichofanyika mjini Nyalikungu wilayani humo.

Wajumbe hao walisema serikali imekuwa ikiwalipa madiwani kiinua mgongo
pindi muda wao wa miaka mitano unapomalizika lakini kwa wajumbe wa
mamlaka hizo huwa hawapewi hali ambayo hawaelewi sababu ya msingi ni
ipi.

“Serikali imekuwa ikiwalipa kiinua mgongo madiwani wanapomaliza muda
wao baada ya kutumikia kwa kipindi cha miaka mitano lakini kwa wajumbe
wa Mamlaka za miji mdogo hakuna kitu kama hicho hapa mie nashindwa
kuelewa kuna sababu ipi?’Alihoji Paschal Nkamu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Robert Mugeta, alisema
utaratibu wa kuwalipa wajumbe wa Mamlaka ya Mji wanapomaliza muda wao
haupo katika maelekezo ya serikali tangu hapo awali na hadi sasa
hawana waraka wowote unaowaelekeza juu ya malipo hayo ya kiinua mgongo
kwa wajumbe hao.

“ kulipwa au kutolipwa kiinua mgongo kwa wajumbe kunategemea waraka
kutoka serikalini utaoamua na kama utawahi kuja na maelekezo muhimu
basi wajumbe hao wataarifiwa mara moja lakini hadi sasa hakuna
maelekezo yoyote yakuwalipa kiinua mgongo”Alisema.

Alisema kuwa kwa ufahamu wake kupitia nyaraka mbalimbali na pia
amekuwa akihudhuria vikao mbalimbali vya serikali vya kujadili viinua
mgongo huwa nasikia habari za wabunge na madiwani tu.

Naye Mbunge wa jimbo la Maswa Mashariki,Slvester  Kasulumbayi(Chadema)
alishauri kwa kuwa suala hilo haliko kisheria hivyo ni vizuri mchakato
wakauanzisha kuanzia huku chini hadi ufike katika bunge ambacho ndicho
chombo cha kutunga sheria.

‘wajumbe mimi nashauri tusichoke kupigia kelele suala hili kwani hata
hizi sheria huwa zinaanzia huku chini kabla ya kufika bungeni na
kutungiwa sheria sasa na sisi tuanze mchakato kwa kulipeleka suala
hili serikalini kwa maandishi wakati huo naomba tuwe nasubira hadi
hapo serikali itakapotoa uamuzi kuhusu malipo hayo kwani ni
muhimu”alisema..

0 Response to "WAJUMBE WA BARALAZA LA MAMALAKA MIJI MIDOGO WAIOMBA SERIKALI KUWALIPA KIINUA MGONGO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.