Habari za hivi Punde

TANZANIA YAENDA KUTIBU UGONJWA WA EBOLA AFRIKA MAGHARIBI

Tanzania imetuma timu ya madaktari bingwa watano wa magonjwa ya mlipuko ikwemo Ebola katika nchi ya Siera Leoni watakaoenda kusaidia kutoa huduma kwa wagonjwa wa ugonjwa huo hatari wakata taifa hilo na mataifa mengine ikiwemo Laiberia yakiendelea kukubwa na ugonjwa huo ikiwa ni mkakati wa nchi katika kushiriki katika nguvu ya mataifa ya umoja wa Afrika kudhibiti ugonjwa huo.
Akitoa taarifa hiyo katika wizara ya afya nchini mganga mkuu wa serikali Dk. Donani mmbando amesema timu ya madaktari hao itaondoka nchini tarehe 8 octoba mwaka huu kwenda kushirikiana na madaktari wengine katika nchi ya Liberia na kuongeza kuwa Tanzania inatambua tishio la ugonjwa huo na ipo tayari kuendelea kutoa msaada katika mataifa yaliyoathirika ili kuhakikisha wagonjwa wa ugonjwa huo wanapona kupunguza kasi ya maambukizi. 
Dk. Mmbando licha ya kukiri jithada zilizokwisha kuchukuliwa na serikali katika kujiandaa kupambana na ugonjwa huo amekiri bado nchi haina maabara daraja la tatu yenye uwezo wa kugundua mgonjwa mwenye ugonjwa huo na mpaka sasa kinachoweza kufanyika nchini ni kupima joto la mwili pekee na kubaini kuna hatua za kuboresha maabara yenye darala la kukaribia la tatu iliyopo mkoani Mbeya. 
 
Baadhi ya madaktari hao wanaoondoka nchini leo licha ya kukiri kuogopa ugonjwa huo wamesema hatua ya maambukizi iliyofikiwa hivi sasa ni lazma kila daktari mwenye uwezo wa kutibu ugonjwa huo aamke na kutoa mchango wake katika kudhibiti maambukizi mapya kwani ugonjwa huo hatari hauchagua mipaka na unaweza hata kuingia nchini Tanzania.

0 Response to "TANZANIA YAENDA KUTIBU UGONJWA WA EBOLA AFRIKA MAGHARIBI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.