MKOA
wa Shinyanga bado unaendelea kutikisa kwa mauaji yanayosaikiwa kusababishwa na
imani za kishirikiana nchini baada ya wanawake wawili kutoka familia moja,kuuawa
kikatili
baada ya kuchinjwa kwa panga na watu wasiofahamika wakati wakijiandaa
kula chakula cha usiku.
Kwa
mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alisema
tukio hilo limetokea Oktoba 14 mwaka huu saa mbili usiku katika kitongoji cha
Nanzilo kijiji cha Ihugi,kata ya Lyamidati tarafa ya Nindo wilaya ya Shinyanga
vijijini.
Kamanda
Kamugisha aliwataja wanawake hao
waliouawa kikatili kuwa ni Dilu Tungu(80) na mtoto wake
Bunya Mihangwa(45),ambao ni wakazi wa kitongoji hicho.
Kamanda
Kamugisha alisema wanawake hao wakiwa wanajiandaa kula chakula cha usiku na
wanafamilia wenzao ghafla walivamiwa na watu watatu wasiofahamika
kisha kuanza kuwakata kwa panga sehemu mbalimbali za miili yao kabla ya
kuitimisha unyama huo kwa kuwachinja
shingo hadi wakapoteza maisha.
Chanzo
cha tukio hilo kinatajwa kuwa ni imani za kishirikina kwani kuna mwanamme
aitwaye Bwanya Mlyashimba(40) (ambaye anashikiliwa na polisi) mkazi wa Ihugi
alikuwa akiwatuhumu marehemu hao kwamba walimroga yeye na kusababisha akose
nguvu za kiume na kwamba walimroga
mama
yake Hollo Mahangwa aliyefariki dunia mwaka 2013.
Bwanya Mlyashimba anashikiliwa na jeshi la polisi,huku Jeshi hilo likiendelea na jitihada za kuwatia mbaroni watuhumiwa wengine.
Bwanya Mlyashimba anashikiliwa na jeshi la polisi,huku Jeshi hilo likiendelea na jitihada za kuwatia mbaroni watuhumiwa wengine.
0 Response to "WANAWAKE WAWILI MKOANI SHINYANGA WACHINJWA SHINGO ZAO NA WATU WASIFAHAMIKA"
Post a Comment