Habari za hivi Punde

WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA UPENDO NA KUONDOKANA NA MAUAJI HARAMU YA WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI (ALBINO))

MKURUGENZI wa Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges ,Alexander Kazimil akitoa nasaha.


MWITO umetolewa kwa jamii kujenga hamasa ya upendo miongoni mwao itakayoibua ari ya kutetea wanyonge sambamba na kuzingatia maadili ya dini hali itakayosaidia kuliondoa Taifa katika matukio ya kufedhehesha kama ukatiri wa mauaji ya Albino na vikongwe.

Mwito huo ulitolewa juzi na Mkurugenzi wa shule ya Sekondari ya Anderleck ya Mjini Kahama Alexander Kazimiri katika mahafali ya 12 ya shule hiyo yaliofanyika mjini Kahama huku wahitimu 158 wakihitimu kidato cha nne katika shule hiyo. 

 VIJANA wa shule ya Rocken Hill Academy walikuwepo katika mahafari hayo na kutoa burudani wa ngoma ya utamaduni wa Mtanzania.


Mkurugenzi huyo alilaani ukatiri huo huku akidai sababu kubwa ya ukatiri huo ni ufinyu wa elimu hivyo kuomba jamii iwekeze zaidi katika sekta hiyo huku akiomba kila Mtanzania kutimiza wajibu wake sambamba na  walimu wakihakikisha wakiweka kipaumbele katika mafundisho yao kupinga ukatiri huo hatua itakayosaidia kulinusuru Taifa na fedheha hiyo.
Alisema msisitizo  ukiwekwa mashuleni ana uhakika vitendo hivyo ambavyo mbali na kufedhehesha Taifa pia ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu vitatoweka huku akisisitiza jamii kubadirika kwa sasa na kumwogopa Mungu kwani vitendo hivyo ni vya kinyama na vinapaswa kukemewa na kila mtu ili viweze kutoweka kabisa.

MGENI rasmi katika Mahafari hayo,Afisa Mkuu wa Ugawaji Rasilimali kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania;Masozi Nyirenda,akitoa nasaha.


  “Taasisi ya Anderlek  tunalaani vitendo vya mauwaji ya albino vinavyofanywa na watu wenye roho mbaya ,kwani ni kinyume na haki za binadamu, watu hawamuogopi Mungu kwa kuweka kando vitabu vyake vitakataifu,badala yake wameweka mbele mapanga,visu na mashoka kuwakata miguu na mikono hata kuwatoa uhai kaka na dada zetu,”Alisema Kazimir
Hivyo aliomba kila kada iwajibike kwa kuhakikisha inatokomeza mauaji hayo,kwa waumini wa dini mbalimbali kushinda katika nyumba zao za ibada,askari polisi na vyombo vya sheria navyo vitimize wajibu wao kwa wakati muafaka na kwa haki hali itakayosaidia kutokomeza mauaji hayo ya watu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.. 

HII ni moja ya Burudani iliyotolewa katika Mahafari hayo.


Aidha aliiomba jamii kurudisha utamuduni wa zamani wa  kujisomea vitabu mbalimbali kwa muda mwingi ili kuweza kuweza kuongeza maarifa hali itakayo saidia vijana wanahitimu elimu za juu kukabiliana na mataifa mengine katika ushindani wa soko la Ajira Duniani. 
Alisema  jamii nyingi za Kitanzania hazina utamaduni wa kujisomea Vitabu na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa kupitwa na mambo mengi yanayoendelea katika dunia hii ya sasa na kuongeza kuwa wanafunzi wakati wakisubiri matokeo yao ni bora wakawa wakijisomea vitabu mbalimbali ili kuongeza maarifa zaidi.

WAHITIMU hao nao walitoa burudani


Mkurugenzi huyo alidai kwa sasa Taifa limepoteza mwelekeo mkubwa hususani kwa vijana ambao kwa kiasi kikubwa hawasikilizi hata vipindi vya Radio vyenye kuwaongezea maarifa zaidi ya kukabiliana na maisha katika jamii ndio maana wamebakiwa kuwa walalamikaji juu ya ugumu wa maisha. 
Kwa upande wake Mgeni Rasmi katika mahafali hayo Afisa Mkuu Ugawaji Rasilimali  kutoka mamlaka ya Elimu Tanzania Masozi Nyirenda alisema kuwa kwa sasa Wanafunzi wanatakiwa kuangalia masomo yatakayowajenga katika mbinu za kujiajiri na si kusubiri kuajiriwa. 
Masozi aliwataka pia Wanafunzi wawapo majumbani wawe mabalozi wa kuweza kuripioti matukio  ya maovu yanayotendeka katika jamii kwani na wao ni mojawapo katika sehemu ya jamii ambayo inatakiwa kuhakikisha Taifa linaendelea kuwa na amani.

0 Response to "WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA UPENDO NA KUONDOKANA NA MAUAJI HARAMU YA WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI (ALBINO))"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.