Habari za hivi Punde

WANAFUNZI WAASWA KUSOMA MASOMO YENYE TIJA YANAYOENDANA NA SOKO LA AJIRA.

WANAFUNZI wa shule za Sekondari mkoani Shinyanga wametakiwa kusoma masomo yenye tija yatakayokwenda sambamba na soko la ajira hasa katika wakati huu mgumu wa kuajiriwa.
Kauli hiyo ilitolewa na  mkuu wa
wilaya ya Kahama Benson Mpesya kwenye maafali ya kumaliza kidato cha nne kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kishimba iliyopo katika halmashauri ya mji wa Kahama.
Katika mahafali hayo Mpesya aliyewakilishwa na Afisa uhamiaji wilayani humo Zacharia Misana alisema ili kupata ajira ni kusoma masomo ya sayansi yatakayoweza kuwapa ujuzi wa kupata maarifa ya kujiajiri wenyewe badala ya kutegemea ajira.
Mkuu wa shule hiyo Melkisedeck Choya alisema usomaji wa masomo ya sayansi katika shule hiyo ni mgumu kutokana na kuwa na maabara ambayo haijakamilika pamoja na serikali kufanya jitihada za kuyakamilisha kwa haraka.
Choya alisema pamoja na changamoto hiyo shule ya sekondari Kishimba, ilikuwa ikikabiliwa na uporomokaji mkubwa wa maadili, na kwamba hivi sasa jitihada za kuirudisha kwenye nidhamu zinaendelea kwa ushirikiano wa walimu, wazazi na jamii inayowazunguka.
Katika mahafali hayo jumla ya shilingi milioni moja na nusu zimechangwa na wazazi waliokuwa wamehudhutia pamoja na mifuko 19 ya saruji iliyotolewa na walimu wa shule hiyo, ili kukabiliana na tatizo la maabara zisizokamilika.

0 Response to "WANAFUNZI WAASWA KUSOMA MASOMO YENYE TIJA YANAYOENDANA NA SOKO LA AJIRA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.