Habari za hivi Punde

WAUMINI WA KANISA LA KKKT WAMETAKIWA KUISOMA KATIBA PENDEKEZO.



WAUMINI wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-KKKT-mission ya Tabora  wametakiwa kuisoma rasimu ya katiba iliyopendekezwa na kuielewa ili waweze kuipigia kura ya maoni.
 
Akizungumza  katika ibada ya Jumapili Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la KKKT mission ya Tabora, Patrick Kiula, alisema waumini wamekuwa ni watu wavivu wa kusoma na hivyo kubaki kulalamika tu.
Kiula alisema waumini wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika masuala ya jamii ikiwemo katika kuisoma rasimu ya katiba na kuipigia kura ili kuweza kuwa na  katiba inayowajali Watanzania.
Alisema kwa sasa rasimu ya katiba iliyopendekezwa inapatikana hivyo kinachotakiwa ni waumini kuitafuta kwa hali na mali na kuisoma ili kuweza kutambua vitu vilivyopendekezwa kwenye rasimu hiyo.
Mchungaji KIULA aliwataka waumini hao kuacha tabia ya uvivu wa kujisomea vitu vya msingi hasa vya kijamii ili kuhakikisha kuwa wanakwenda sambamba na watu wengine  kuliko kukaa bila kufahamu kinachoendelea katika nchi yao.

0 Response to "WAUMINI WA KANISA LA KKKT WAMETAKIWA KUISOMA KATIBA PENDEKEZO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.