Habari za hivi Punde

MENO YA TEMBO YAKAMATWA HUKU WATU TISA WAKISHIKILIWA NA JESHI LA POLISI

WATU wadhanwao ni  majangili katika pori la akiba Maswa waliofanya tukio la  kutungua
helkopita ya kampuni ya Mwimba Holding Limited na kusababisha kifo cha
Rubani,  Rodgers Charvis  raia wa Uingeleza ambaye alikuwa
akitekelezamajikumu yake jeshi la polisi limefanikiwa kuwakamata
wahusika 9 pamoja na bunduki 29  ikiwemo  meno ya tembo matatu.

Akiongea  jana na waandishi wa habari mkoani Simiyu, Kamanda wa polisi
mkoani hapa Lazaro Mambosasa alisema kuwa jeshi hilo limefanikiwa
kuwakamata watuhumiwa 9 ambao walihusika na tukio la kuangusha
helkopita pamoja na kusababisha kifo cha Rubani wa ndege hiyo.

Alisema kuwa jeshi la polisi lilifanyamsako mkali ambao ulisababisha
kuwakamata watuhumiwa wawili ambao ni ShijaMjika (38) na Masasi
Mandogo (48) ambao walifanikisha kukamatwa kwawatuhumiwa wengine saba
waliohusika katika tukio hilo.

Alisema baada ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao wawili walitaja na
kuonesha meno mawili ya tembo yenye kilogram 31aliyeuawa  januari 29
mwaka huu ambayo walikuwa wameyaficha kwenye daraja katika kijijicha
Itaba.

Alibainisha kuwa baada ya kukamatwa kwa watuhumiwahao wawili jeshi la
polisi liliwahoji na kukiri kuhusika na tukio hilo nakumtaja ambaye
alifyatua risasi kwenye helkopita  ambaye ni Dotto Pangali (41) ambaye
alikamatwaakitaka kujaribu kutoroka kuelekea mkoa wa Shinyanga.

Kamanda mambosasa alisema kuwa baada ya kukamatwakwa mtuhumiwa huyo
alikiri kutungua helkopita hiyo kwa kutumia Bunduki yaReffle yenye
namba 7209460 CAR Na 63229 ambapo inamilikiwa na Mange Balumambaye kwa
sasa anashiliwa na jeshi la polisi .

Kamanda huyo alisema kuwa baada ya upekuzi wa kinakwenye mji wa Dotto
Pangali kulipatikana na Bunduki aina ya Reflle yenye namba3478 CAR Na
458 ikiwa na risasi 6 inayomilikiwa na Nghomango Jilala ambaye
amekimbia na anaendelea kutafutwa na jeshi hilo.

Alifafanua kuwa katika oparesheni hiyo piawalifanikiwa kukamata
watuhumiwa wengine ambao ni Njile Gonga (28),Iddi Mashaka(49),Mwigulu
Kanga (40),Mapolu Njige (50)wote wakai wa kijiji cha Sungu ,DottoHuya
(45)mkazi wa kijiji cha Itaba pamoja na Mange Balum(47)mkazi wa kijiji
cha Itaba wilayani Meatu.

“katikamsako huo tumefanikiwa kukamata bunduki 27 pamoja na Risasi
141 ambazozinawamiliki ambao wamekuwa wakizikodisha silaha hizo kwa
majangili kwenda kuulia tembo katika hifadhi za taifa na tumekamata
Shotgun 11 na risasi 44,Raflle 10 na risasi zake 105 pamoja na
magobole 6 yakiwa na risasi 2”alisema.

0 Response to "MENO YA TEMBO YAKAMATWA HUKU WATU TISA WAKISHIKILIWA NA JESHI LA POLISI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.