Habari za hivi Punde

WANANCHI KUCHANGIA UJENZI WA MAHAKAMA ZA MWANZO




 WATUMISHI  wa idara ya mahakama mkoani Shinyanga wametolewa hofu ya kuhakikisha wananchi  wanashirikishwa ili kuweza  kuboresha miundombinu ya majengo  kama wafanyavyo kwenye sekta zingine.

Hayo yamesemwa   na mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Rufunga   kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyka kwenye viwanja vya mahaka mkazi wilaya nakuhusisha wadau kutoka maeneo mbalimbali wakiwemo viongozi wa madhehebu ya dini.



Rufunga amesema kuwa kumekuwepo na miundombinu chakavu hasa kwenye mahakama  za mwanzo pindi mvua ikinyesha hasa msimu huu wa masika kesi zimekuwa zikiahirishwa  hali hiyo inaendelea kuwepo msongamano wa  watuhumiwa magerezani  kwa kuchelewa kwake.



Naye hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama  ya mkoa wa Shinyanga  Rahimu Mushi alisema kuwa  baadhi ya mahakama za mwanzo miundombinu yake ni mibovu  aliiomba serikali kuwashirikisha wananchi kuboresha  miundombinu hiyo kwa kuchangia kama wanavyochangia kwenye sekta zingine.

Amesema  hivi  sasa mahakama imeongeza ufanisi wake katika utendaji kazi  kwa mwaka 2015 kulikuwa na  mashauri  400 ya muda mrefu lakini mpaka sasa kuna mashauri yasiyozidi 130   bado kumekuwepo na changamoto  ya  baadhi ya wananchi kushindwa kujitokeza mahakamani kutoa ushahidi kwa dhana kuwa watafungwa.


Naye mwakijilishi kutoka kwa mawakili wa kujitegemea mkoani hapa Jacob Msomi alipokuwa akitoa taarifa yake mbele ya mkuu wa mkao amesema kuwa tabia ya  msemo kuwa  polisi ukienda ni bure nakutoka ni pesa hilo likomeshwe ikiwemo kukamata kamata hovyo  na kubambikia kesi ndio inayofanya  hata magereza kuwepo msongamano.

0 Response to "WANANCHI KUCHANGIA UJENZI WA MAHAKAMA ZA MWANZO"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.