Habari za hivi Punde

DC SHINYANGA ATOA AGIZO MHANDISI WA MANISPAA KUWEKWA RUMANDE

MKUU wa  wilaya  ya  Shinyanga  Josephine  Matiro  ametoa  amri  ya kumuweka  ndani  mhandisi  wa ujenzi wa manispaa ya Shinyanga  Saimon  Ngagani ,  kutokana  na kukaidi  agizo lake  la kufanya  maandalizi  mapema  ya  shughuli  za  kuchimbia  mapipa  ya  kuweka  taka  nyepesi  katika  maeneo  mbalimbali  ya manispaa  hiyo. 

Akizungumza na  baadhi ya   wananchi  katika  stendi  ya  mabasi  ya zamani  wakati wa kuweka mapipa hayo ,mkuu wa wilaya alisema zoezi  hilo lilitakiwa lifanyike saa  1.30 asubuhi lakini wamelazimika kufanya saa 3.30  kutokana  na uzembe uliofanywa na injinia  ambaye alipewa  kazi ya  kuandaa  kokoto  na  mchanga mapema matokeo  yake  hakufanya  hivyo.

  Kwanza aliagizwa  na mkurugenzi  wa manispaa  hiyo  Lewis  Kalinjuna  kufanya  maandalizi  mapema ya vitu vinavyotakiwa kwenye  kazi  ya kuweka  mapipa  ya taka  nyepesi,matokeo  yake mpaka  leo  asubuhi  hakuna  kilichofanyika hak una kokoto  wala simenti eneo la kufanyika kazi  huu ni uzembe , mkuu wa kituo  uko wapi kamata  huyu muweke  ndani”aliagiza mkuu wa wilaya.
 
Hata  hivyo  mkuu  wa  wilaya aliwataka  wananchi kuyatumia kwa kuweka taka  nyepesi huku  akiwatahadharisha wafanyabiashara  wa vyuma  chakavu, kuwa  makini na watu  wanaowauzia  vyuma  hivyo  na kuwafichua watakao  yaharibu  na kwenda  kuuza  wakibainika  hatua  kali  zitachukuliwa  dhidi  yao.
 
Alisema  iwapo  mazingira  yatakuwa katika  hali  ya  usafi  jamii  haiwezi kukumbwa  na  ugonjwa  wa kipindupindu  na  magonjwa  mengine ,nakusisitiza kuwa suala  la  usafi linatakiwa  kuwaendelevu  kuanzia sehemu  wanayoishi, kwenye  biashara  na maeneo  yanayowazunguka.
 
 Awali  akijitetea   mhandisi huyo  wa manispaa    Ngagani alisema tatizo  lililofanya achelewe kufanya  maandalizi  ni kutokana na  kukosa  fedha za kununua kokoto  na  simenti  na kulazimika  kuanza  kuomba  kwa wadau  na kufanikiwa kupata muda  ukiwa umeenda.
 
Kwa  upande  wake ofisa  afya  wa manispaa  hiyo  Elly  Nakuzerwa  alisema  jumla  ya mapipa 50 ya kuweka  taka  nyepesi  yametolewa  na wadau mbalimbali wa maendeleo,  ikiwa  ni kuhakikisha mji unakuwa katika hali ya  usafi na kujiepusha  na mlipuko  wa  magonjwa kikiwemo  kipindupindu.
Aliwatahadharisha  wananchi kutoweka  mabaki  ya vyakula  kwenye  mapipa  hayo  na kuwataka  kuzingatia usafi kwa  kila  mmoja, ambapo  atakayebainika anatupa uchafu  hovyo atatozwa faini  ya  papo kwa papo sh  50,000 na akishindwa anapelekwa mahakamani.


0 Response to "DC SHINYANGA ATOA AGIZO MHANDISI WA MANISPAA KUWEKWA RUMANDE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.