Habari za hivi Punde

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU CHATOA ELIMU YA RASMU YA PILI YA KATIBA.






KITUO cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC)  kimetoa elimu ya Rasmu ya pili ya  katiba  kwa wananchi wa kata ya kitangili mjini shinyanga ili wananchi hao wapate kuelewa pamoja na kujitokeza kupiga kura pale Rasmu hiyo itakapo rudishwa mikononi mwa watanzania kama imekidhi vigezo na maoni waliyoyapendekeza

Akitoa elimu kwa wakazi hao kwenye mkutano wa hadhara mwanasheria wa Kituo hicho Jonsoni John alisema kuwa lengo la kutoa elimu  ya Rasmu ya pili ya katiba ni kukuza uelewa kwa watanzania iliwapate kujua nini maana ya katiba hali ambayo itachangia kupata katiba safi ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ambayo itaongoza maisha ya watanzania na vizazi vyake vyote.


John alisema baadhi ya watanzania hawaifahamu katiba ya nchi hivyo wao kama kituo cha sheria na kutetea haki za binadamu wameona vyema kutembelea baadhi ya mikoa hapa nchi  kutoa elimu hiyo kwa wananchi pamoja na kugawa vitabu na vipeperushi vinavyo elezea Rasmu ya pili ya katiba hali ambayo itawapanua kimawazo na kutambua mambo gani ya muhimu yanafaa kuwepo katika katiba mpya

Amesema  Bunge  la Rasmu ya pili ya katiba lililopo mjini Dodoma ambalo hivi karibuni litafanya kazi ya kupitia maoni ya watanzania pamoja na kufanya maboresho yaliyopendekezwa juu ya kuundwa kwa katika mpya na Rasmu hiyo itakapo rudishwa kwa watanzania ,itawakuta watanzania wanaupeo wa kutosha na hivyo kuichambua kwa makini kama mapendekezo yao muhimu yamefanyiwa kazi.

 Akizungumza kwenye mkutano huo mkurugenzi msaidizi wa Kituo hicho Ezekiel Masanja amesema  kuwa Watanzania ndio wenye ridhaa ya kukubali ama kukataa Rasmu hiyo ya pili ya katiba ipitishwe au isipitishwe na hivyokuamua kuendelea kutumia katiba ya zamani ya mwaka 1977 endapo kama wakiona mapendekezo yao ya msingi hayapo

 Katika mkutano huo wananchi walikuwa wanaulizwa maswali juu ya Katiba na Rasmu ambapo asilimia kubwa walionekana kutokuwa na uelewa wa vitu hivyo viwilli na mara baada ya kupewa elimu hiyo walifunguka vichwa vyao na kuyatambua mambo muhimu yanayofaa kuwemo katika Rasmu ya pili ya katiba ambayo ndio itaunda katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania

0 Response to "KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU CHATOA ELIMU YA RASMU YA PILI YA KATIBA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.